Friday, January 31, 2014

MZEE GURUMO AFUNGUKIA SKENDO ZA DIAMOND

Mayasa Mariwata na Shani Ramadhan
MSANII mkongwe wa muziki wa dansi
Bongo, Muhidini Gurumo ambaye kwa sasa
amestaafu, amefungukia skendo ya kuwa na
mademu wengi inayomuandama Nasibu
Abdul ‘ Diamond ’ .
Nasibu Abdul ‘ Diamond ’ .
Akipiga stori na Ijumaa hivi karibuni maeneo
ya Ilala jijini Dar, Mzee Gurumo alisema :
“ Diamond ana nidhamu sana ila vile
anavyotamba jukwaani na kudatisha
mashabiki hapo ndipo balaa linapokuja,
watoto wa kike wenyewe wanaanza
kujisogeza kwake .
Mzee Muhidini Gurumo .
“ Pamoja na skendo za mademu
zinazomuandama , siwezi kumshusha
thamani, ana haki ya kujiopolea mwanamke
yeyote anayempenda, yeye kama
mwanaume rijali wakati mwingine ni vigumu
kujizuia na vishawishi hivyo.”

GP

No comments:

Post a Comment