Wednesday, February 05, 2014

Bond Bin Sinnan: mi kwa upande wangu siipendi siasa ila siwezi washangaa hao walioingia katika siasa kwa sababu ni moja kazi pia

Baada ya baadhi ya wasanii wakubwa kuingia kwenye siasa iki ndio amekisema mtangazaji wa kipindi cha “Action and cut“ bond bin sinnan

Mi kwa upande Wangu siipendi siasa ila siwezi washangaa hao walioingia katika siasa kwa sababu Ni moja ya kazi pia. Siasa Ni ofisi za watu wanaoziweza ofisi zao na kazi hizo so kwa wana sanaa kujiunga na siasa maanake wanajaribu kazi nyingine kama tulivyoona hapo awali wasanii kama Joseph Mbilinyi Mr 2, Joseph Haule profesa J, Selemani Msindi Afande Sele, Roma na Nakaya wao wamejiunga na Chadema kwa nyakati tofauti na hakuna alie shangaa wala kuwachukia na pia Vicky Kamata na Kapteni Komba na wao walijiunga na CCM kwa nyakati tofauti na hakuna alie shangaa pia hivyo hata hawa Wa filamu watu wasushangae sana na wawape sapoti endapo watataka kugombea nyadhifa mbalimbali. Na haya ukiangalia nje watu kama Govinda, Mithuni Chakrabot na Amithab Batchan kwa Bollywood wamewahi kuingia ndani ya siasa na Haya Hollywood pia Anord Schwazniger pia ametoka katika siasa juzi tu. Hi yo hawapaswi kuhukumiwa au kuhojiwa kwa maamuzi yao ya kuangalia ofisi nyingine na pia wana impact kubwa katika kuitangaza nchi pia Ni jambo zuri kwa wao kuitangaza siasa ya nchi yetu nje zaidi...

No comments:

Post a Comment