Muongozaji wa filamu mwenye jina kubwa nchini Bond Bin Sinnan ambae anatokea jiji la Mwanza ameshindwa kuficha hisia zake baada ya kumaliza kazi ya kuongoza filamu mpya ya Wastara Juma iki ndio amekisema
"Nilitamani
kuufanyia kitu mkoa nilikotokea, nilitamani kuonyesha ulimwengu mwanza
iko vipi na nashukuru nimefanya hivyo kupitia filamu ya Last Decision ..
nimeonyesha location nzuri zote mfano Bismarock, sehemu za kutengeneza
mapanki (mabaki ya sangala baada ya kutowa minofu) nyumba za milimani
zilizojengwa juu ya mawe na kati kati ya jiji la mwanza.. kwa kweli
nimefurahi sana kufanya kazi na Wajey Film na Freedom fighter Film.
Imani yangu kubwa watanzania watafurahia filamu hii pia nimefurahi kuona
vipaji vipya toka mwanza na pia nimefurahi kufanya kazi na Hemed kwani
alivaa nilivyomwambia na pia hakuvaa hereni wala kuweka marangi kwenye
nywele amecheza uhalisia mzuri kama baba wa mtoto mmoja na mume Wa
Wastara. Naimani wapenda filamu watapata burudani nzuri kupitia filamu
hii"
No comments:
Post a Comment