Sunday, July 20, 2014

Bond Bin SINNANN:Nilitamani kuufanyia kitu mkoa nilikotokea, nilitamani kuonyesha ulimwengu mwanza iko vipi na nashukuru nimefanya hivyo kupitia filamu ya Last Decision ..

Muongozaji wa filamu mwenye jina kubwa nchini Bond Bin Sinnan ambae anatokea jiji la Mwanza ameshindwa kuficha hisia zake baada ya kumaliza kazi ya kuongoza filamu mpya ya Wastara Juma iki ndio amekisema
"Nilitamani kuufanyia kitu mkoa nilikotokea, nilitamani kuonyesha ulimwengu mwanza iko vipi na nashukuru nimefanya hivyo kupitia filamu ya Last Decision ..

 nimeonyesha location nzuri zote mfano Bismarock, sehemu za kutengeneza mapanki (mabaki ya sangala baada ya kutowa minofu) nyumba za milimani zilizojengwa juu ya mawe na kati kati ya jiji la mwanza.. kwa kweli nimefurahi sana kufanya kazi na Wajey Film na Freedom fighter Film. 

 Imani yangu kubwa watanzania watafurahia filamu hii pia nimefurahi kuona vipaji vipya toka mwanza na pia nimefurahi kufanya kazi na Hemed kwani alivaa nilivyomwambia na pia hakuvaa hereni wala kuweka marangi kwenye nywele amecheza uhalisia mzuri kama baba wa mtoto mmoja na mume Wa Wastara. Naimani wapenda filamu watapata burudani nzuri kupitia filamu hii"


No comments:

Post a Comment