Saturday, February 22, 2014

MASTAA WAKOMALIA BUNGE LA KATIBA

BAADHI ya mastaa wa Bongo Movies
wameamua kujitoa kinaga ubaga kwenda
Dodoma kwa ajili ya kuweka msisitizo kwa
wabunge wa Bunge la Katiba juu ya maslahi
ya kazi zao .

Taarifa zinaeleza kuwa, miongoni mwa
mastaa ambao wamekita kambi pande za
Dodoma ni pamoja na Rais wa Shirikisho la
Sanaa Nchini , Siamon Mwakifwamba pamoja
na Kulwa kikumba ambaye
amefafanua uwepo wao mjini humo :
“ Tunataka kuhakikisha bunge hili la katiba
linatuthamini katika suala zima la kutetea
maslahi ya kazi zetu , huu ni muda wa
wasanii kuamka, tuzalishe fedha kulingana
na jasho letu , ” alisema Dude.

No comments:

Post a Comment