Saturday, January 04, 2014

Wastara ni mfano wa kuigwa:Yuster Nyakachara

Mmiliki wa kampuni ya Eagle Intertainment Yuster Nyakachara amesema Wastara Sajuki ni muigizaji anaefaa kuigwa kwa kazi zake na busara zake na jinsi alivyokuwa jasiri kumuuguza marehemu mume wake.

Amesema jamii ilitegemea kwakua ni maarufu basi angemtelekeza mume wake lakini haikua hivyo amekua karibu yake mpaka umauti umemfika

Nyakachara amesa Wastara anajitaidi sana kwenye kazi zake kwani ni mkongwe anaefanya vizuri na kampuni yake binafsi tofauti ba wakongwe wengine ambao mpaka leo wanacheza filamu za kushirikishwa

Ameongeza pia ata kwa mavazi wastara amekua mfano wa kuigwaa kwani anavaa nguo za heshima zenye kustili mwili wake

Yuster hivi karibuni anatarajia kuachia filamu yake ya kwanza Majuto si Hasira akiwa amewashirikisha wasanii wenye majina bongo movie

No comments:

Post a Comment