Saturday, May 31, 2014

Katika gari hilo walikuwaGEOGRE TYSON AFARIKI DUNIA KWA AJALI MBAYA YA GARI AKITOKEA DODOMA

 Marehemu Geogre Tyson pichani hapa alikuwa yupo kijiji cha Chilonwa Chamwino kwenye utoaji wa madawati katika shule ya msingi Chaula iliyopo Dodoma. Baada ya kumaliza shughuli hii huku akiwa kama producer wa The Mboni Show mauti yalimkuta majira ya saa 12 jioni masaa 4 tu toka Kuanza safari ya kurudi Dar es Salaam maeneo fulani hivi kama unataka kukaribia GAIRO mjini.

 Katika gari hilo walikuwa watu 8 ila yeye pekee ndio aliyepoteza mauti na wengine kupata majiraha mwilini pamoja na dereva wa gari hilo. Kwa sasa mwili wa marehemu umehifadhiwa mjini Morogoro katika hospital ya mkoa Morogoro, asubuhi hii mwili unategemewa kusafirishwa kurudi Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment