Saturday, March 08, 2014

DAVINA AMSHAURI WASTARA

BAADA ya staa wa filamu za Kibongo ,
Wastara Juma kutoa shukurani kwa wasanii
wenzake zilizotafsiriwa kama anajitabiria
kifo chake , msanii mwenzake , Halima
Yahaya ‘ Davina’ ameibuka na kumtaka
asikate tamaa .
Halima Yahaya ‘ Davina ’ .
Alisema alishtuka baada ya kuona maelezo
gazetini ( Ijumaa Wikienda) ambayo Wastara
alimpongeza kama rafiki mwenye mchango
na hakujua kama anathamini na kukumbuka
vitu watu walivyomfanyia ila kikubwa
amemtaka asikate tamaa kwa yote
yaliyomtokea.
“ Asikate tama , mitihani tumeumbiwa
wanadamu, tunapaswa kuishinda, ” alisema
Davina.

No comments:

Post a Comment