Monday, January 13, 2014

Sara apata gonjwa la ajabu

MSANII wa sinena za Kibongo ambaye amejikita kwenye nyimbo za Injili, Sara Mvungi amejikuta kwenye wakati mgumu kutokana na kusumbuliwa na maradhi ya tumbo bila kujua chanzo wala ugonjwa husika.

Akizungumza na paparazi wetu, Sara alisema katika hali ya kutaharuki tatizo hilo lilipoanza alihisi labda anasumbuliwa na ugonjwa wa ‘typhoid’ lakini alipokwenda hospitali hakukutwa na tatizo ingawa tumbo linazidi kumuuma.

“Nashindwa kuelewa nasumbuliwa na nini mpaka sasa, hali yangu ilikuwa mbaya sana. Nilipoenda hospitali sikuonekana na tatizo kutokana na kile kinachonisumbua, Mungu ataniponya,” alisema Sara.

GP

No comments:

Post a Comment