Tuesday, November 19, 2013

Mwanaume aua watu wawili na kisha kujiua yeye kwa risasi jijini Dar leo

Mtu mmoja ambaye bado hajafahamika jina lake amewaua watu wawili kwa kuwapiga risasi ndani ya gari na kujeruhi mmoja kisha naye akajiua kwa risasi asubuhi hii jirani na Baa ya Wazee iliyopo Ilala, jijini Dar es Salaam!
 
Inadaiwa kuna gari ilikua inatoka ndani ya geti kutoka ikiwa na dereva mwanaume, abiria mwanamke mbele, na abiria wengine wawili wakiwa seat ya nyuma.
 
Pembeni hapo kulikua na jamaa kasimama. Inadaiwa alishushwa hapo dakika chache toka katika tax, walipotokeza abiria hao kupitia gari yao alitoa silaha yake na kupiga risasi gari akilenga zaidi abiria wa mbele pande zote kisha na nyuma. Baada ya kumaliza hapo muuaji huyo naye alijipiga risasi na kufariki hapo hapo.
 
Dereva na abiria wake wa mbele wamefariki dunia, huku abiria wa nyuma mmoja mama mtu mzima kajeruhiwa na risasi mgongoni na dada mwingine kajeruhiwa kwa kupigwa risasi mguuni.

Source: GPL & Jamiiforums

No comments:

Post a Comment