Friday, July 04, 2014

CATHY: USTAA KWENYE NDOA NI TATIZO

MSANII maarufu katika tasnia ya filamu Bongo, Sabrina Rupia ’Cathy’ amewataka wasanii wenzake kutofanya ustaa kwenye ndoa zao kwani ndiyo chanzo cha kuvunjika kwa ndoa nyingi.


Akipiga stori na paparazi wetu, Cathy alisema kabla ya kuolewa lazima uwe na utayari wa kuolewa na kujuana kwa undani zaidi na mwenzio kabla ya kufanya uamuzi pia usiweke neno kuachika katika ndoa kwa sababu tu unaweza kupata mwingine.
“Uvumilivu ndiyo nguzo muhimu katika ndoa, unapojifanya staa na kuishi maisha ya kistaa katika ndoa, mambo yanaharibika kabisa,” alisema Cathy huku akikataa kutoa mifano ya walioachika kwa kuendekeza ustaa katika ndoa akidai wanajijua.

No comments:

Post a Comment