Wednesday, July 02, 2014

BONGO MUVI WAFUNIKA KWA MAUNO

MASTAA  wa kike katika tasnia ya filamu Bongo Sabrina Rupia ‘Cathy’, Salma Salim ‘Sandra’ na Rose Ndauka juzi walikuwa kivutio kwa wananchi waishio maeneo ya Kinondoni jijini Dar baada ya kushindana kuzungusha nyonga.
                                  Staa wa filamu Bongo Sabrina Rupia ‘Cathy’.


 Mastaa hao walifanya tukio hilo katika sherehe za kuwasimika ukamanda wa vijana Tawi la CCM Bwawani ililopo maeneo hayo wakati walipopagawa na vikorombwezo vya Msaga Sumu katika wimbo wa taarab.
 
                                              Staa wa filamu Bongo, Rose Ndauka.

 Dah kumbe mastaa wetu wana fani nyingi, angalia mauno yale utafikiri hawana mifupa sehemu za kiunoni,” alisikika akisema njemba moja lililokuwa likishuhudia shoo hiyo ya bure.


                                                 Staa wa filamu Bongo, Salma Salim ‘Sandra’.

chanzo globalpublishers 
 

No comments:

Post a Comment