Friday, December 13, 2013

“Kutongozwa kwa mwanamke ndio faraja kwani tumeubwa kuchaguliwa na si kuchagua“Riyama Ally

Mcheza filamu za kitanzania Riyama Ally amesema hakuna ukweli wowote kuwa wataarishaji wote wa filamu nchini wanatabia za kutongoza wasanii wa kike ili wawape nafasi kwenye filmu zao.

Akiongea na blog hii amesema mapenzi siku hizi imekua kawaida na mdada unaweza kutongozwa popote sio kwenye sanaa tu na kuongeza kuwa kutongozwa ni faraja kwa mwanamke kwani wameubwa kuchaguliwa na sio kuchagua ila unaetongozwa unatakiwa kusema hapana kwa watu wasio lazima katika maisha yako

“kutongozwa kwa mwanamke ndio faraja kwani tuliumbwa kuchaguliwa na sikuchagua  ila wewe unaetongozwa unatakiwa kusema hapana kwa watu wasio lazima katika maishayako“

Amesema wasanii wa kike wanatakiwa kuvaa nguo zenye maadili zitakazo wafanya wapewe heshima ata na waandaaji wa filamu

No comments:

Post a Comment