Friday, November 08, 2013

Baada ya kua kimya kwa muda mrefu sasa nimerudi rasmi kwenye tasnia ya filamu

Nilikua kimya muda mrefu kwa matatizo ambayo wengi mnayajua ila sasa nimerudi kwenye tasnia yangu ya filamu na hivi karibuni natarajia kuachia filamu yangu mpya inaita Shaymaa(alama) na siku zote na amini moyo wa mwanadamu siku zote unatamani kuwa na furaha,moyo ukikosa furaha unaweza kufanya jambo usilotarajia au ukamkera mwingine,lengo lako ni kutafuta amani na furaha,mwangaza wa kuiona kesho yenye furaha na hiyo ndio Shaymaa

hadithi ya Shaymaa nimeandika mwenyewe lakini muongozo na kuiongoza ni Leah(lamata),pia nimewashilikisha Salma Nisha na Yusuph Mlela na wasanii wengine

chini ni picha baadhi wakati tunaandaa filamu hii
Naomba mashabiki wangu wote mkae mkao wa kula maana nimetoa kitu kizuri naamini mtajifunza kitu kupitia mimi

No comments:

Post a Comment