Friday, August 22, 2014

ESHA BUHETI GONJWA GONJWA, TUMUOMBEENI

MUIGIZAJI aliyelamba tuzo ya Muigizaji Bora wa Kike katika Tamasha la Zanzibar Festival Film ‘ZIFF’ mwaka huu, Esha Salim Buheti hali yake siyo nzuri na anahitaji maombi ili apone kutokana na kusumbuliwa na tatizo la uvimbe kwenye kizazi.
 katika Hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni jijini Dar, Esha alisema, alifikishwa hospitalini hapo juzi Jumatano akiwa na hali mbaya kufuatia ‘kuendesha’ ile mbaya. “Nilifikishwa hapa nikiwa na hali mbaya, nilikuwa ‘naendesha’ sana hadi kufikia hatua ya kuishiwa nguvu, ilibidi wanichukue vipimo ili kujua tatizo

“Baadaye wakaniambia nina uvimbe kwenye kizazi na UTI, yaani dah! Naomba Mungu anisaidie na naomba mashabiki wangu pia waniombee nipone,” alisema Esha.

No comments:

Post a Comment