Tuesday, April 08, 2014

Wastara:“marehemu Kanumba na mume wangu Sajuki ni mashujaa wa bongo movie waliotutoka ikiwa bado tunawitaji

Mcheza filamu nyota wa Tanzania Wastara Juma amesema marehemu Steven Kanumba na mume Juma Kilowoko (sajuki) ni mashujaa wa filamu waliotangulia mbele ya haki ikiwa bado wanaitajika

Wastara amesema vifo vya wasanii vimetokea vingi tena kwa kufatana kwenye tasnia ya filamu na muziki na kwamba kwa upande wake amepata pigo kubwa sana alipompoteza mume wake kipenzi Sajuki

“yani nimeanza upya kabisa sanaa najiona niko tofauti sana maana mume wangu nilimzoea sana kwenye utaarishaji wa filamu zetu ata hivyo nashukuru mungu najitaidi kupambana na soko “

Amesema Kanumba amejitaidi kututanga kimataifa na anaamin kama angekuwepo basi tungepiga atua sana japo waliopo wanajitaidi kufata nyayo zake

No comments:

Post a Comment