Sunday, November 10, 2013

Wastara:Hizi ndio sababu za kumuweka Salma Nisha kwenye filamu ya Shaymaa

Msanii wa kike katika filamu za kibongo Wastara Sajuki amesema kwenye filamu yake mpya ya Shaymaa amemuweka Salma Nisha kwa kua ni muigizaji mwenye uwezo mkubwa na anajua anachokifanya

Amesema sababu nyingine stori ilikua inataka mtu anaefanana nae kawa rangi na kimwili hivyo akaona Nisha ndio chaguo sahihi

Kwa upande wake Niasha amesema amefurai kucheza filamu hiyo kwani alikua anampenda Wastara tangu akiwa kidato cha pili hivyo ametimiza ndoto yake ya muda mrefu

Aidha amesema kwenye filamu hiyo amecheza kama Shaymaa na kuwaomba mashabiki wainunue kwa wingi itakapotoka ili waone alichokifanya

Filamu ya Shaymaa inatarajiwa kutoka mwishoni mwa mwezi huu na wamo Yusuph Mlela,Salma Nisha na waigizaji wengine wengi

No comments:

Post a Comment