Thursday, March 23, 2017

RACHEL YUPO HONEYMOON MOROGOROOO!

 MWIGIZAJI wa kike katika tasnia ya filamu Swahilihood Rachel Bitulo yupo mkoani Morogoro kikazi akirekodi filamu inayokwenda kwa jina la Honeymoon huku yeye akiwa kinara wa sinema hiyo akishirikiana na staa kibao wa Mkoani humu amesema Rachel Bitulo staa wa filamu ya Nimekosea wapi?
 “Kwa sasa nipo busy sana kwani narekodi filamu ya huku Morogoro ni kazi nzuri sana najua itazidi kuniweka pazuri zaidi katika tasnia ya filamu Bongo sinema yenyewe inaitwa Honeymoon,”.
Rachel amesema kuwa filamu hiyo imetayarishwa na mtayarishaji wa Mkoani Morogoro anaitwa Bravo ambaye amejitambulisha kwa jina moja tu, pia katika filamu hiyo yupo mwwigizaji mwingine anayejulikana kwa jina la Idrisa Makupa aka Kupa sambamba na wasanii nyota kutoka Moro.

No comments:

Post a Comment